Fahamu malengo ambayo mfumo wa WAKALA NAMI umeweka ili kuboresha na kukuza huduma za uwakala Tanzania.
Kuipa sekta ya uwakala njia ya kutumia teknolojia kufanya biashara kwa urahisi, uwazi na kwa kasi bila kutegemea mfumo wa karatasi au simu za kawaida.
Kujenga mtandao mpana wa mawakala wakuu na wadogo ili kuongeza upatikanaji wa huduma na kufikia maeneo mengi zaidi nchini.
Kuwezesha mawakala kupata zana na huduma zinazorahisisha ukuaji wa biashara zao na kuongeza mapato kwa kuwahudumia wateja wengi zaidi.
Kuhakikisha wateja wanapata huduma haraka, salama, na bila kukwama kutokana na upatikanaji wa float kwa wakati.
Kutoa taarifa za miamala zinazoonekana papo hapo ili kupunguza makosa, migogoro na kuongeza uaminifu kati ya mawakala na wateja.
Kuunda mazingira ya kidigitali yenye usalama wa juu, yanayowezesha biashara kuendelea bila vikwazo na kwa uadilifu.
Wasiliana nasi kwa maswali, maombi ya huduma, au usaidizi wowote unaohitaji katika shughuli zako za uwakala.